Maandalizi ya mashindano ya mbio za Safari Rally ambayo yameratibiwa kuandaliwa baina ya tarehe 24 na 27 Juni mwaka huu yanakaribia kukamilika. Akizungumza wakati alipoandamana na wanahabari katika ukaguzi wa mkondo utakaotumiwa, afisa mkuu wa mbio za Safari Rally Phineas Kimathi alifichua kuwa kituo cha kuhudumia magari kinachojengwa katika Shule ya Mafunzo ya Huduma ya Wanyamapori ya Naivasha, kinakaribia kukamilika.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN
Follow us on Twitter: https://twitter.com/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1news
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#KBCchannel1 #KBCsports #KBClive